• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

RASIMU YA WILAYA

HALMASHAURI YA WILYA YA MWANGA

 

RASIMU  YA  WILAYA  YA  MWANGA 

 

UTANGULIZI.

UTAWALA  .

Wilaya ya Mwanga ilianzishwa mwaka 1979 na ni mojawapo kati ya Wilaya sita (6) za Mkoa wa Kilimanjaro.  Kiutawala Wilaya ya Mwanga ina Tarafa 5 ( Kuna  Tarafa  moja  mpya  ya  Kindoroko  ambayo  haijaanzishwa rasmi, ikianzishwa  Wilaya  itakuwa  na Tarafa  6). Wilaya ina Kata 20, Vijiji 72 , Mji Mdogo  wa  Mwanga na kuna  jumla ya  Votongoji  273. Kati    ya  Vitongoji  273  Vitongoji  12  viko  katika  Mji  Mdogo  wa  Mwanga  na  Vitongoji   261  viko  katika  Vijijini  72  vya  Wilaya..

MIPAKA   YA  WILAYA.

Wilaya  iko  kati  ya  Nyuzi 30 25’’  na  Nyuzi 30 55’’  Kusini  mwa  Ikweta, na iko  kati  ya  370 25’’  na Nyuzi 370 58’’  Mashariki  mwa  Mstari  wa  ’’Greenwhich’’.Wilaya ya Mwanga imepakana na Wilaya ya Moshi kwa upande wa Kaskazini, nchi jirani ya Kenya upande wa Mashariki, Wilaya ya Same upande wa Kusini na Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara upande wa Magharibi.

 

  Eneo  la  Wilaya na  Mwinuko  wa Nchi.

Wilaya  in ukubwa  wa  Kilometa  za mraba  2,641 ,kati  ya  hizo  eneo la  Kilometa za   mraba   2,558.6   ni  la  Nchi   kavu  na  zilizobakia  Kilometa za   mraba   82.4   ni  za  maji  ya  Nyumba  ya  Mungu ( Km2 56)  na  Ziwa  Jipe (Km2 26.4 ). Wilaya  iko kati  ya  Mita  700  -2,212  juu  ya  usawa  wa  Bahari.

 

    1.4 .Hali ya Hewa

Hali ya hewa wilayani kwa asilimia kubwa ni  ya ukame.  Kuna misimu miwili ya mvua, Vuli ambayo huanza mwezi wa Octoba hadi mwezi Disemba na Masika ambayo huanza mwezi Machi hadi Juni.  Wilaya  huwa  na  Upepo  mkali  na  mkavu unaovuma  tokea  upande  wa  Mashariki  mwa  Wilaya  kuelekea   Magharibi. Kiwango cha joto huwa ni kati ya nyuzi joto 140 C  kwenye mwezi Juni na Julai na miezi mingine huwa ni nyuzi joto  320 C . Wilaya  ina Kanda  2  Kuu  za  Kilimo  , Kanda  ya  Nyanda  za Chini Mashariki  na  Chini  Magharibi  na Nyanda  za Juu. Nyanda  za  Chini  kiwango  cha  mvua  kwa  mwaka  huwa  kati  ya  400mm- 600mm.  na  Nyanda  ya  Juu  kiwango  cha  mvua  kwa  mwaka  huwa  kati  ya  800mm- 1,200mm.

IDADI   YA  WATU.

Muhtasari  wa  Idadi  ya  Watu –Matokeo  ya  Sensa  ya Watu  na Makazi  Toka  mwaka  1978-2012.

Mwaka

Idadi  ya  Watu

Ongezeko

Asilimia (%) ya Ongezeko

Idadi  ya Kaya

Wanaume

Wanawake

Jumla.

1978

35,621

38,909

74,530

 -

-

13,551

1988

46,362

50,642

97,004

22,474

30.15

17,487

2002

55,327

59,818

115,145

18,141

18.70

24,326

2012

63,199

68,243

131,442

16,297

14.15

29,875

 

 

 

HUDUMA ZA KIUCHUMI.

 

  • Shughuli  kuu za  kiuchumi.

 Asilimia 85 ya wananchi wanaishi vijijini.  Uchumi wa wilaya unategemea sana kilimo, ufugaji, uvuvi na sehemu ndogo wanajishughulisha na biashara ndogo ndogo.  Mazao makuu ya biashara yanayolimwa ni Kahawa,na Mkonge . Mazao ya chakula ni Mahindi, Maharage, Ndizi, Mihogo, Viazi vitamu na Mpunga.

 

2.1. Kilimo

Wilaya ya Mwanga ni wilaya ya kilimo na ufugaji na kwa kiasi kidogo uvuvi na biashara.  Asilimia 85 ya Wananchi wa Mwanga wanaishi vijijini kwa kutegemea zaidi kilimo na ufugaji.Eneo linalofaa kwa kilimo ni ha 44,300, kati ya hizo hekta 7,409 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji.  Jumla ya eneo linalolimwa na kumwagiliwa maji ni hekta 3,648, kati ya hizo hekta 2,230 humwagiliwa kwa sikimu za umwagiliaji zilizopo kati  ya eneo la hekta 5,280 na hekta 1,418 humwagiliwa na Ndiva  kati  ya  eneo  la  hekta 2,209. Hekta 36,891 zinategemea kilimo cha maji ya mvua.

 

2.5  Mifugo

      Ufugaji unakwenda sambamba na kilimo kwani unachangia Wananchi kuinua kipato chao.  Wapo zaidi ya ng’ombe 51,010 wa kisasa wakiwa 12,260, mbuzi 36,449 wa kisasa wakiwa 410, kondoo 22,240, nguruwe 497, punda 4,943, sungura 196, kuku 98,726, bata 11,901 na ngamia 6. Yapo malambo 9, majosho 13 na Vituo vya mifugo 9 kwa ajili ya kuboreshaufu.

 

 

2.6  Maliasili na Mazingira

.

Jina  la Msitu

Aina ya Msitu

Mahali   Ulipo/Vijiji

Ukubwa-Ha.

Hadhi  ya Msitu

Mramba
Msitu  wa  Asili
Kifaru; Kisangiro and M
Kwanyange

3,355

Msitu  wa  Hifadhi.
Kirongwe
Msitu  wa  Asili
Kiverenge; Ngullu; and Sofe.

1,758.4

Msitu  wa  Hifadhi
Kindoroko
Msitu  wa  Asili
Ngujini; Chanjale; Sofe; Ndorwe; Chomvu and Kilomeni.

885

Msitu  wa  Hifadhi
Minja
Msitu  wa  Asili
Vuchama Ngofi

520

Msitu  wa  Hifadhi
Kamwala  1
Msitu  wa  Asili
Vuchama Ndambwe; Mfinga; Mkuu; Shighatini ; Kighale; and Kirongaya.

119.25

Msitu  wa  Hifadhi
Kamwala 11
Msitu  wa  Asili
Songoa  and Ngujini.

292

Msitu  wa  Hifadhi.
Kileo
Msitu  wa  Asili
Kileo

191

Msitu  wa  Hifadhi
Mbachi
Msitu  wa  Asili
Vuchama Ngofi

97.4

Msitu  wa  Hifadhi
Mbochiro
Msitu  wa  Asili
Kifaru na Kisangiro.

588

Msitu  wa  Hifadhi
Total

7,806.05


 

 

2.8  Miundombinu/Barabara.

Wilaya ya Mwanga pamoja na kuwa na Barabara kuu ya lami yenye urefu wa km 63.5, reli km. 50 kutoka Dar es Salaam kwenda Kaskazini pamoja na nchi jirani. Wilaya ina  jumla  ya  Barabara zisizo  za Lami zenye jumla  ya kilometa  744.8  , kati ya  hizo  Kilometa 7.5 ni  za Lami, 294  ni  za changarawe na  kilometa 443.3 ni  za udongo.  Wakala wa Barabara (Tan Roads) wanahudumia km 191 na Wilaya inahudumia km. 609.8

 

 

 

 

2.9   Reli.

Kuna Reli inayopita  Wilayani Mwanga yenye urefu wa kilometa 55 inayotoka Moshi kuelekea Tanga na Dar-es- Salaam. Kwa sasa hivi Reli haitumiki  kwa  kusafirisha  abiria  wala   mizigo kutokana  na  kuwepo  kwa  vyombo  vingi  vya  usafiri  wa abiria  na mizigo  na  vinvyochukua  muda mfupi  kwenda   sehemu fulani  ukilinganisha  na  treni, hivyo  wasafiri  na  wasafirishaji  mizigo  hutumia  usafiri  wa barabara  na kufanya  usafiri   wa treni  kukosa  abiria   na mizigo.

2.10 Ushirika

Katika suala la kupambana na umaskini, wilaya imeweka nguvu kubwa katika kuanzisha na kuimarisha vyama vya akiba na mikopo (SACCOs). Wilaya kwa sasa ina SACCOS 21 zenye wanachama 4,963 ambao wamechangia hisa zenye thamani ya Tsh. 76,713,000/-, akiba Tsh. 278,157,000/- na amana za Tsh. 23,706,400/-..Katika kuendeleza miradi yao ya kiuchumi wanachama wa SACCOs wameweza kukopa kupitia vyama hivyo, jumla ya Tsh. 1,049,597,500/- na tayari wamesha rejesha Tsh. 1,098,812,600/-. Kiasi kilichobakia mikononi mwa wanachama ni Tsh. 310,784,900/-. Hata hivyo mahitaji bado ni makubwa zaidi.

2.11 Madini /Viwanda.

      Wilaya ya Mwanga ina  Kiwanda  kimoja  kikubwa  cha Kilimanjari- Bio-Chem  kilichopo  kijiji  cha  Kifaru  kinachotengeneza  bidhaa  za  ‘’Spirit ‘’( 96  % Ethanol) tokana  na Mollases  na  kimeajiri  Watumishi  130  kwa  sasa. Wilaya pamoja na kuwa  na aina ya madini , haina Viwanda vya uchimbaji madini ya aina yoyote kwa hivi sasa kinachofanya kazi.Kuna madini ya Shaba kwa kiwango kidogo na wachimbaji waliopo ni wadogo wadogo na kiwango cha uzalishaji hakijajulikana. Pia kuna madini aina ya Jasi ambayo hayajaanza kuchimbwa na kiwango kilichopo bado hakijulikani. Kuna jumla ya Mashine za kukoboa na kusaga 73 na viwanda vidogo vodogo vya useremala na  uchomaji vyuma 23  ambavyo vinatoa ajira kwa  watu karibú 3,000.

2.12 Uvuvi.

Uvuvi ni shughuli  muhimu inayowapatia mapato  wakazi wanaokaa kandokando ya Bwawa la Nyumba ya Mungu , wastani wa Kilo 476.48  huvuliwa kwa mwaka katika Bwawa hilo zenye  thamani  ya  Tshs.  1,511,330,200. Kuna jumla  ya Wavuvi 660 na  mitumbwi midogo ( Canoes) 378 .

2.13 Ufugaji Nyuki.

Shughuli za ufugaji Nyuki na uzalishaji wa Asali na Nta ni kidogo sana katika Wilaya ya Mwanga  kuna Mizinga ya asili 2,500 na ya  Kisasa  135  inayozalisha wastani wa Kilo 720 kwa  mwaka  yenye  thamani ya Tshs.5,760,000.

 2.14  Biashara 

 Wilaya ina  idadi ya biashara zifuatazo:- Baa  55, ‘’Grocery’’  18, Maduka ya rejareja  1,523, ‘’Viosk’’  45, Bucha 41, Mikahawa  14, ‘’Garage’’ 2,Maduka ya rejareja na jumla 5, Hotel 3- Kindoroko Mountain Lodge- Kisangara, Mhako Hotel- Usangi  na  Anjela Inn Hotel Mwanga Mjini. Motel 2-Mwanga Mjini,  Nyumba za kulala wageni 16, na kuna Vituo vya Mafuta  5 vinavyofanya kazi, Mwanga Mjini 2, Kifaru  1, Kisangara  1 na Mgagao 1.

 

2.15 Nyumba za kufikia Wageni na Viongozi.

Wilaya ina ‘’Rest House’’ moja ya kufikia Viongozi Wakuu wa Serikali ya Serikali Kuu na nyingine moja ya Halmashauri.

3.0 HUDUMA ZA JAMII

    3.1 Rasilimali Za Maji

Wilaya ya Mwanga ina Ziwa Jipe ambalo lina ukubwa wa kilometa za mraba 26.4 na likiwa limekaa katika mpaka wa nchi ya Kenya na Tanzania na Bwawa la Nyumba ya Mungu ambalo lina ukubwa wa kilometa za mraba 140.

Vyanzo  vikuu  vya  Maji  kwa Vijijini  ni  Chemu  chemu  za  asili, Ziwa  Jipe,  Bwawa  la  Nyumba  ya  Mungu  na Mto  Pangani.

3.2  ELIMU.

  3.2.2 Elimu ya msingi

Uandikaishaji  katika  Shule  za Msingi mwaka  2012.

  Wilaya ina Shule za Msingi 113, kati ya hizo 109 ni za Serikali na 4 ni za watu binafsi Kuna jumla ya wanafunzi 30,005 kati yao 15,209 wavulana na wasichana 14,796.    katika  Shule  za Serikali   29,825, Wavulana 15,115 na  Wasichana 14,710. Wastani wa mahudhurio shuleni ni  asilimia 98.01 . Kati Shule 113 za Msingi kuna Shule maalum 18 za walemavu kama ifuatavyo:- Shule ya Elimu Maalum kwa  Viziwi 1 (Mwanga), mchanganyiko kitengo cha Viziwi 1- Mramba, na Elimu Jumuishi 16.

 

  3.2.3 Elimu  ya  Sekondari.

Shule za sekondari zipo 41, kati ya hizo 25 ni za Serikali na 16 ni za binafsi, kati ya hizo Shule zenye Kidato cha I-VI  ni 13 , Shule 5 zikiwa ni za Serikali  na 8 za binafsi.  Pia kuna Vyuo 3 vya Ufundi Stadi na Chuo kimoja cha binafsi cha Ualimu

3.2.4 Vyuo  vya  Elimu  ya  Ufundi  (VETA).

Kuna   Vyuo  vya  VETA  6  ,  3  ni  vya  Serikali  na 3  ni  vya  binafsi.

 

3.3 AFYA

 Vituo vya Tiba Vilivyopo.

Aina/Mmiliki

Idadi

Hospitali  za  Serikali

1

Hospitali  za  Taasisi/ Binafsi

0

Vituo  vya  Afya  vya  Umma

5

Vituo  vya  Afya  vya  Taasisi/Binafsi

1

Zahanati  za  Umma

40

Zahanati za  Taasisi/ Binafsi

5

3.4   MAENDELEO  YA  JAMII.

  Mfuko wa Wanawake (WDF)

Mfuko huu uko rasmi kwa ajili ya kuwakopesha wanawake ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi hatimaye kujikwamua na janga la umaskini.

 Vikundi mbalimbali

Wilaya ya Mwanga ina vikundi (CBOS)  390, Asasi za kijamii 5.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA WA MAGARI 12 September 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGA KURA October 02, 2025
  • Tangazo la ukarabati wa vibanda September 03, 2025
  • TANGAZO LA KAZI June 03, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • RAS - KILIMANJARO ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI, HALMASHAURI YA WILAYA YA MWANGA

    September 25, 2025
  • Kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima

    September 04, 2025
  • Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata wapewa mafunzo

    August 04, 2025
  • DC MUNKUNDA AONGOZA KONGAMANO LA MWAKA LA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (NGOs)

    June 18, 2025
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa