• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

AFISA AFYA WILAYA YA MWANGA; "WANANCHI CHUKUENI TAHADHARI JUU YA MLIPUKO WA KIPINDUPINDU"

Posted on: September 21st, 2018

Siku za karibuni imeripotiwa kuwa, umetokea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, kwa baadhi ya maeneo ya Halmashauri ya Moshi iliyoko Mkoani Kilimanjaro, na baadhi ya maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro iliyoko Mkoani Manyara. Mpaka sasa maeneo yaliyoripotiwa kuwa na mlipuko wa ugonjwa huo ni 6, ambapo maeneo hayo ni TPC, Mabogini na Kahe kwa Mkoa wa Kilimanjaro na Msitu wa Tembo na Chemchemi kwa Mkoa wa Manyara.

Kaimu Afisa Afya wa Wilaya ya Mwanga, Ndg. Happynus Pilula amesema, japokuwa ugonjwa huo haujatokea Wilayani Mwanga, Wananchi hususani wananchi wanaoishi pembezoni mwa mto Pangani na maeneo ya bwawa la Nyuma ya Mungu, wanapaswa kuchukua tahadhari mapema ili wasipatwe na ugonjwa huo.

Ndg. Pilula amesema, mpaka sasa Wilaya imeshachukua jitihada mbalimbali ili kuhakikisha tahadhari ya mapema, inachukuliwa dhidi ya mlipuko wa ugonjwa huo. Jitihada zilizochukuliwa mpaka sasa ni pamoja na, kutoa elimu kwa wananchi, wauzaji wa vyakula na maji kuhakikisha wanafuata taratibu za afya, kusisitiza wananchi kuchemsha maji ya kunywa na kila mwananchi ahakikishe ana choo na kitumike. Jitihada zingine zilizofanywa ni, Idara ya afya imesha agiza dawa za dharura na zipo tayari ili kuhakikisha kuwa, endapo mlipuko utatokea, wananchi wanapata matibabu ya haraka.

Hata hivyo Kamati ya Halmashauri ya kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu, imeweza kuketi, na kuweka mikakati madhubuti itakayowezesha kabiliana na hali yoyote itakayopelekea mlipuko wa ugonjwa huo.

Sambamba na hilo, wananchi wote wanasisitizwa, kutoa taarifa mara moja pale wanapohisi uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika maeneo yao na kuhakikisha kuwa, wanawapeleka wagonjwa kwenye vituo vya afya mara tu wanapoona dalili za ugonjwa huo.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa