• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA MWANGA LAPITISHA BAJETI YA TSH. BILIONI 31.3

Posted on: January 26th, 2022

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga leo tarehe 26 Januari, 2022 kwa kauli moja, wamepitisha mpango wa bajeti ya Halmashauri kiasi cha shilingi za kitanzania bilioni 31.3 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Akizungumza kwenye mkutano wa Baraza hilo Mhe. Salehe R. Mkwizu ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri amesema, bajeti hii inakwenda kuakisi maendeleo ya Halmashauri pamoja na wananchi wa Mwanga.

Mhe. Mwenyekiti amesema kuwa, bajeti hii vipaumbele vyake vikuu ni pamoja na kuboresha mazingira ya utendaji kazi kama kushughulikia stahiki za watumishi na kuongeza vitendea kazi, kuboresha na kuimarisha miundombinu ya mifugo na uvuvi, kusimamia utekelezaji wa sheria ya mipango miji na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kama vifaa tiba, kupunguza vifo kwa mama na mtoto, ukarabati wa miundombinu ya afya.

Vipaumbele vingine ni kuboresha miundombinu ya mifugo na uvuvi, kuongeza uzalishaji wenye tija kwa mazao ya kilimo kama korosho, katani na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji, ununuzi wa zana za kilimo, kuongeza ukusanyaji wa mapato na kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kuboresha kanzidata ya walipa kodi na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kwa kudhibiti utoro na mimba.

Ameendelea kusema kuwa, bajeti imezingatia mambo mbalimbali kama utekelezaji wa ilani ya chama tawala, miongozo ya Serikali ikiwamo mpango wa maendeleo endelevu 2030, Dira ya Taifa 2025, kukuza fursa za ajira na uboreshaji wa miundombinu, kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na ununuzi wa samani kwa ajili ya majengo ya utawala na viongozi wa Halmashauri, kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Sambamba na hotuba yake hiyo, Mwenyekiti amesema kuwa, bajeti inayokwenda kuisha ya mwaka 2020/2021 ilikuwa na changamoto mbalimbali kama ushiriki mdogo wa wananchi kwenye kutekeleza miradi ya maendeleo, fedha za miradi kutotolewa ama kutolewa kidogo tofauti na malengo, uwezo mdogo wa Halmashauri kuchangia miradi mingi ya maendeleo, kutopatikana kwa wakati vifaa vinavyohitajika vinavyotoka kiwandani hivyo kusababisha ucheleweshaji wa baadhi ya hatua za miradi, upungufu wa watumishi katika idara mbalimbali.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa