• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA MAKISIO YA BAJETI KIASI CHA TSH. BILIONI 36.78

Posted on: January 19th, 2023

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, leo limepitisha rasimu ya bajeti ya Halmashauri yenye makisio ya Tsh. Bilioni 36.78. Baraza hilo la madiwani limepitisha bajeti hiyo huku wakikiri kwamba, ni bajeti ambayo imegusa maeneo yote ya msingi kuanzia ngazi ya jamii hadi uchumi wa mwananchi wa chini wa Wilaya ya Mwanga.

Akiwasilisha bajeti hiyo mbele ya Mkutano wa Baraza hilo la Madiwani, Mhe. Salehe R. Mkwizu, ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga na Diwani Kata ya Shighatini amesema kwamba, bajeti hii imebeba viapumbele mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutekeleza na kusimamia yaliyomo kwenye ilani ya chama tawala.

Mhe. Mkwizu pia amesema, pamoja na mambo mengine, bajeti hii imezingatia mambo mengi ikiwa ni pamoja na mpango wa maendeleo wa Taifa, mwongozo wa bajeti wa 2023/2024, kuboresha mazingira ya utendaji kazini, matumizi bora ya ardhi, upatikanaji bora wa huduma za afya, kuongeza uzalishaji wa mazao yenye tija, kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato na kuongeza ufaulu katika shule za msingi na sekondari.

Mambo mengine ambayo bajeti hii imezingatia ni kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi, kuboresha miundombinu ya mifugo na uvuvi, kudhibiti mapato ikiwa na pamoja na kuongeza kasi katika kukusanya mapato ya Serikali, kuboresha miundombinu pamoja kukuza fursa za ajira.

Aidha, katika hotuba yake ameendelea kusema kwamba, Halmashauri ya Mwanga, kwenye makusanyo ya mapato ya ndani imekadiria kukusanya kiasi cha Tsh. Bilioni 2.9 kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato vilivyoko ndani ya Halmashauri.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa