• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

HIZI NDIZO KAMATI MPYA ZA BARAZA LA MADIWANI (W) MWANGA

Posted on: August 16th, 2018

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, leo limeketi na kufanya uchaguzi wa viongozi na wajumbe watakaounda, kamati mbalimbali ambazo zipo kisheria.

Uchaguzi huo ambao umefanyika chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, Mhe. Theresia P. Msuya umefanikiwa kuunda jumla ya kamati nane ambapo kila kamati ina Mwenyekiti wake. Kamati hizo ni Kamati ya Fedha, Uongozi, na Mipango ambapo Mwenyekiti wake ni Mhe. Theresia P. Msuya, Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Mwenyekiti ni Mhe. Jeremia Shayo, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Mwenyekiti ni Mhe. Enea Mrutu.

Kamati zingine ni pamoja na Kamati ya Maadili, ambapo Mwenyekiti wake ni Mhe. Baraka Maradona, Kamati ya Ukimwi, Mwenyekiti wake ni Mhe. Fihiri Mvungi, Bodi ya Ajira ambayo mjumbe wake ni mmoja ambaye ni Mhe. Mwalim Ziad, ALAT wajumbe wawili ambao ni Mhe. Rodgers Msangi na Mhe. Kuria Msuya na kamati ya mwisho ni Ardhi yenye wajumbe wawili ambao ni Mhe. Aisha H. Salema na Mhe. BokaBakari S. Kuria.

Aidha Kamati hizi ambazo huwa zinaundwa na kuchagua uongozi wa kuziongoza, uchaguzi wake huwa unafanyika kila mwaka mpya wa fedha, hivyo kwa mwaka huu wa fedha 2018/19 uundaji wa hizo kamati umefanyika leo. Sambamba na kuunda kamati hizo, Waheshimiwa Madiwani wamefanya uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ambapo, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Mhe. Fihiri Msuya amechaguliwa tena kuendelea kuwa Makamu M/Kiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga.

Baada ya kamati kuundwa na viongozi wa kamati kupatikana,Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri aliwashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa kuweza kushiriki vizuri kwenye kuwachagua Wajumbe na Wenyeviti wa kila kamati.
Mheshimiwa Mwenyekiti amewasisitiza na kuwaomba wajumbe wa kila kamati kuhakikisha kuwa, wanashiriki kwenye vikao ambavyo wao ni wajumbe ili waweze kutoa maamuzi sahihi na yenye tija kwa taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa