• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

HONGERA AFISA ELIMU MSINGI KWA KUWAJALI WALEMAVU

Posted on: March 7th, 2018

HONGERA AFISA ELIMU MSINGI KWA KUWAJALI WALEMAVU

Ni jambo la kufurahisha pale unapompata mtu mwenye roho ya huruma tena ya kuwajali wenye mahitaji maalumu kama watoto walemavu kwani watoto wenye mahitaji maalum wanahitaji kufarijiwa, kutunzwa na kuthaminiwa.

Hongera hizi zinaenda kwa Afisa Elimu Msingi Ndugu Allan S. Said kwani kwa mara ya kwanza anafanya kitu chenye taswira nzuri ndani ya jamii kwa kuwakutanisha kwa pamoja watoto wenye mahitaji maalum wa Shule za Msingi na kula nao chakula pamoja na kuwapatia zawadi mbalimbali.

Tukio hili ambalo liliwajumuisha watu mbalimbali pamoja na taasisi binafsi lilifanyika kwenye uwanja wa michezo wa C. D. Msuya siku ya jana tarehe 06 Machi, 2018 na kuhudhuriwa na walimu, wananchi, wazazi wa watoto wenye mahitaji maalum pamoja na taasisi mbalimbali kama Benki ya Wananchi Mwanga, Benki ya NMB na taasisi ya Tanesco. 

Akizungumza kwa moyo uliojawa na furaha huku machozi yakimlengalenga kwa namna alivyofurahia jambo hilo Mhe. Theresia P. Msuya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga ambaye pia alikuwa mgeni rasmi alimpongeza sana Afisa Elimu kwa jambo nzuri alilolifanikisha kwa kuwajali watoto hao ambao wanasoma shule zenye mahitaji maalum. Mwenyekiti wa Halmashauri aliendelea kutoa pongezi kwa wote waliotoa michango yao kwa kuhakikisha kuwa watoto hao wanafurahi na kujisikia kuwa nao ni sehemu ya watu wengine. Taasisi zilizotoa michango na zawadi na kuhakikisha kuwa tukio hilo linakwenda vizuri ni pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi, Idara ya Elimu Msingi, Hawa Fashion, Benki ya NMB, Benki ya Wananchi Mwanga, Shirika la Umeme Tanesco Mwanga, Walimu wa shule za Mwanga na watu binafsi.

Akizungumzia juu ya umuhimu wa elimu kwa watoto wenye ulemavu Mhe. Mwenyekiti alisisitiza kuwa kwa sasa ameona kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa shule zenye watoto wenye mahitaji maalum kuwa na walimu wa kutosha na atahakikisha suala hili analisemea kwenye vikao vya Halmashauri ili walimu waliopo kwenye shule hizo wasije wakahamishwa kwani hata hao waliopo hawatoshi kulingana na umuhimu wa watoto hao japokuwa inaonekana kama walimu waliopo kwenye shule za watoto wenye ulemavu ni wengi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri Ndg. Golden A. Mgonzo akizungumza mbele ya watoto hao alisisitiza kuwa watoto wote wanapaswa kupata malezi mazuri pasipo kujali hali zao na ofisi yake iko makini kuhakikisha yeyote atakaye husika katika kuwanyanyasa watoto ndani ya Wilaya yake watapitiwa na mkono wa sheria. Pia aliwaasa wazazi wa watoto wote kuhakikisha kuwa wanafuatilia haki za watoto wao kwenye Ofisi za Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Jamii pale wanapopatwa na matatizo ambayo hawawezi kuyakabili.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa