• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

KITUO CHA AFYA KIRYA KIMEZINDULIWA RASMI

Posted on: November 9th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, leo imezindua rasmi kituo cha afya Kirya na huduma zote za wagonjwa wa nje zimeanza kutolewa. Kituo hicho ambacho kinategemewa kutoa huduma kwa wananchi wa Kirya wapatao 8554, na wananchi wa Wilaya jirani za Same na Simanjiro ya Mkoa wa Manyara, kimekamilika kwa wakati muafaka kutokana na wananchi wa Kata ya Kirya hapo awali kupata huduma hiyo kwenye maeneo yaliyopo zaidi ya kilomita 25.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Ndg. Abdallah Mwaipaya, ambaye amekifungua kituo hicho kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, alisema, kituo hiki ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Mwanga hususani wananchi wa Kata ya Kirya na maeneo ya jirani. Amewataka wananchi hao kuhakikisha kwamba, wanakilinda na kukitunza kituo hicho ili wafaidi huduma ambazo zitakuwa zikitolewa hapo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, Mhe. Salehe R. Mkwizu amesema kwamba, baada ya kituo hiki kukamilika, Baraza la Madiwani kwa pamoja waliridhia kutoa kiasi cha Tsh. Milioni 10 kupitia mapato ya ndani ili ziweze kununua vifaa tiba na madawa, na huduma ziweze kuanza kutolewa kituoni hapo. "Nawapongeza Waheshimiwa Madiwani wangu kwa kukubali kiasi cha Tsh. Milioni 10 za mapato ya ndani zitolewe na ziweze kutumika kununulia madawa na vifaa tiba kwa ajili ya wananchi wa Kirya", alisema Mhe. Mkwizu.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilileta kiasi cha Tsh. Milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la huduma za nje (OPD) na Maabara. Fedha hizo, ndizo zilizotumika kukamilisha majengo hayo na huduma kuanza. Aidha, kiasi kingine cha Tsh. Milioni 250 kimeletwa tena na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji, na huduma ya Mama na Mtoto.



Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa