• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

Mvua zaleta madhara katika Kata ya Kileo

Posted on: May 2nd, 2018

Katika hali isiyo ya kawaida, mvua zinazo endelea kunyesha zimeendelea kuleta madhara makubwa Wilayani Mwanga kiasi cha kupelekea wananchi kupata adha mbalimbali. Pamoja ya kwamba mvua hizi zimenyesha maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Mwanga, Kata ya Kileo ndiyo kata ambayo imeathirika zaidi kulinganisha na maeneo mengine.

Mvua hizi za masika zimepelekea baadhi ya watu kuhama nyumba zao kutokana na nyumba hizo kujaa maji ama kuzingirwa na maji. Mbali na nyumba kujaa maji, vyoo navyo vimetitia ama kujaa maji kabisa, baadhi ya nyumba zimebomoka na kuanguka, visima vya maji vimejaa na baadhi ya barabara hazipitiki kabisa.

Akiwa kwenye ziara ya kujionea namna mvua zilivyo leta athari kwenye jamii, Mbunge wa Jimbo la Mwanga Mhe, Prof. Jumanne Maghembe ameelezwa na uongozi wa Kata kuwa, kwa sasa kuna baadhi ya shule ambazo zimezingirwa na maji hivyo inakuwa ngumu kwa wanafunzi wa madarasa ya chini kuhudhuria shuleni. Shule ambazo zimeathirika na mvua hizi ni za msingi na Sekondari. Shule za msingi ni pamoja na Muungano, Kituri na Kalimani. Shule za sekondari ambazo zimekumbwa na tatizo hili ni Kifaru na St. Joseph.

Madhara mengine ambayo yametokea ni baadhi ya mashamba yenye mazao kuingiliwa na mafuriko hivyo kupelekea mazao kusombwa ama maji kutuama kwenye mashamba hayo. Akizungumza kuhusu athari za mvua za msimu huu hususani kwenye kilimo, Kaimu Mkuu wa Idara ya Kilimo na Umwagiliaji Ndugu Hassan Mamboleo amesema, wakazi wa maeneo yaliyo athirika wahakikishe wanafanya jitihada za kutunza akiba ya chakula walicho nacho kwani mazao mengi yameharibika na hali hii itapelea upungufu wa chakula hususani kwa wananchi wa Kileo.

Naye Kaimu Afisa Elimu, Idara ya Elimu Msingi Ndg. Iyogo Isuja akiwa anazungumzia athari zilizojitokeza hususani kwenye taaluma alisema, baadhi ya wanafunzi wameshindwa kwenda shule kutokana na miundo mbinu ya barabara kutopitika hali ambayo inapelekea wanafunzi hao kukosa masomo. Mbali na baadhi ya wanafunzi kukosa masomo, pia walimu walio mbali na maeneo ya kazi, wanafika shuleni kwa kuchelewa kutokana na miundombinu kutokuwa rafiki kupitika. Hii inapelekea vipindi vya masomo kuanza kwa kuchelewa hivyo baadhi ya vipindi, hususani vipindi vya asubuhi havifundishwi kutokana na adha ya miundombinu ya barabara kutuama maji.

Katika kuhakikisha hatua za awali zinachukuliwa, ili kuepuka madhara ya mlipuko wa magonjwa, Serikali imeshagawa dawa za kutibu maji ya kunywa na wananchi wa Kata ya Kileo wamesha gawiwa dawa hizo. Serikali inawaasa wananchi wote wa kileo kuendelea kuchemsha maji ya kunywa pamoja na kuhakikisha wanatumia dawa za kutibu maji walizo pewa ili wasipatwe na mlipuko wa magonjwa.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa