• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

NACHUKIZWA NA KITENDO CHA WAZAZI KUKATAA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI, MH. MAGHEMBE

Posted on: July 16th, 2018

Mbunge wa Jimbo la Mwanga Mh. Jumanne A. Maghembe amewaambia wananchi wa Kata ya Msangeni kuwa, anachukizwa sana na kitendo cha wazazi kukataa kuchangia chakula cha watoto shuleni.


Mheshimiwa Mbunge ameyasema hayo leo alipokuwa kwenye ziara ya kusikiliza kero za wananchi wa Kata ya Msangeni. Akiongea kwa masikitiko alisema, "Nimepata taarifa kuwa, shule ya Sekondari Msangeni wanaokula chakula cha mchana ni wanafunzi sita tu". Ameendelea kusema, hayuko tayari kuona watoto wanashinda na njaa na atahakikisha kuwa mwezi agosti atarudi kukagua ili kuona kama watoto wanakula chakula shuleni.


Katika kuhakikisha hilo linafanikiwa, Mheshimiwa Mbunge amewaagiza watendaji wa vijiji na kata kuhakikisha kuwa, wanasimamia hili jambo, na kuhakikisha wanakaa na wazazi, na kuwashirikisha ili waone ni kwa namna gani wanaweza kuchangia chakula kwa ajili ya watoto waliopo shuleni.


Pia Mheshimiwa Mbunge ameahidi kuipatia shule ya sekondari Msangeni Kompiuta 45 ambazo zitawasaidia kwenye kujifunza kwa vitendo somo la TEHAMA. Amesema kuwa, hadi kufikia mwezi Octoba, kompiuta hizo zitakuwa zimefika na zitasaidia kuinua taaluma kwenye shule hiyo.


Aidha, Mheshimiwa Mbunge hakuacha kutoa pongezi kwa Serikali ya awamu ya tano kwa kusema, kwa sasa Serikali imeshafanya mambo mengi na makubwa kwa ajili ya wananchi wa Tanzania. Akitaja baadhi ya miradi mikubwa ambayo Serikali imeshafanya ama inaendelea kufanya ni pamoja na ununuzi wa ndege 7 za abiria, ujenzi wa reli ya kisasa, mradi wa kuzalisha umeme uliopo Selous na ujenzi wa barabara nyingi kwa kiwango cha lami ambapo kwa sasa mikoa mingi imeshaungwanishwa kwa barabara za lami.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa