• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAMISEMI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI MWANGA

Posted on: March 11th, 2022

Leo Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. David E. Silinde ametembelea na kujionea miradi mitatu inayoendelea kutekelezwa hapa Wilayani Mwanga. Ziara hiyo ameifanya ikiwa ni sehemu ya mikakati ya serikali kuendelea kukagua na kujionea namna utekelezaji wa miradi hiyo unavyo kwenda.

Miradi aliyotembelea ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Barabara ya Kisangara – Shighatini wenye thamani ya Tsh. Milioni 617.9, mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Kirya ambao kwa hatua za awali umepatiwa kiasi cha Tsh. Milioni 250 na mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Kivisini ambao umepatiwa kiasi cha Tsh. Milioni 470.

Katika ziara yake hiyo, Mhe. Naibu Waziri ametoa maelekezo kwa Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Mwanga na Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Mwanga kuhakikisha kuwa, wanaisimamia miradi hiyo kwa weledi na umakini mkubwa ili iwe na tija kwa wananchi. Amewataka viongozi hao kusimamia vizuri fedha za Serikali na zifanye kazi iliyo kusudiwa. Akizungumzia suala la ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya, Mhe. Waziri amesema kuwa, serikali ilisha ahidi kutoa fedha hizo na zitakuja muda wowote kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akisoma taarifa ya mradi wa Barabara ya Kisangara - Shighatini mbele ya Mhe. Waziri, Mhandisi wa TARURA Wilaya ya Mwanga Ndg. Emmanuel Yohana alisema kwamba, barabara hiyo yenye urefu wa Kilomita 12.3 ujenzi wake umefikia asilimia 47 na itakamilika mwezi juni, 2022.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mwanga Bi. Mwajuma A. Nasombe amesema kwamba, mradi wa ujenzi wa Kituo cha afya ambao unategemea kunufaisha takribani wananchi 8554 mpaka sasa upo katika hatua ya kupandisha kuta na ameahidi ujenzi utakwenda kwa kasi ili kukidhi matakwa ya serikali. Mkurugenzi ameeendelea kusema, hadi kufikia sasa kiasi cha Tsh. Milioni 43 imesha tumika. Pia amesema katika hatua za kujenga majengo ya kituo hicho cha afya, wananchi wameshiriki kwa kuchangia kiasi cha Tsh. Milioni 6 na wadau wa maendeleo wamechangia kiasi cha Tsh. Milioni 4.2.

Aidha katika mradi wa Kivisini Sekondari, mradi ambao upo katika hatua za kupandisha kuta, Mkurugenzi Mtendaji alisema wananchi wa eneo husika wameshiriki vizuri katika hatua zote toka mradi ulipo anza na wamesha changia kiasi cha Tsh. Milioni 8.7. Aliendelea kusema kwamba, Halmashauri kwa hatua za awali imeweza kufanya manunuzi mbalimbali kutoka kiwandani ili kupunguza gharama za vifaa ambavyo vingeweza kununuliwa kwa bei ya juu kutoka kwenye maduka yasiyo ya jumla.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa