• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

SERIKALI YAIPATIA HALMASHAURI YA WILAYA YA MWANGA TSH. BILIONI 1 KWA AJILI YA JENGO LA UTAWALA, KIASI KAMA HICHO KWA AJILI YA JENGO LA HOSPITALI MPYA YA WILAYA

Posted on: March 10th, 2022

Serikali imeipatia Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kiasi cha fedha Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Bi. Mwajuma A. Nasombe katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Teacher Resource Centre (TRC). Amesema kuwa, kwa mwaka wa fedha 2022/2023 serikali imeridhia kutenga kiasi hicho kwa ajili ya kuhakikisha kuwa Halmashauri kwa sasa inakuwa na jengo la utawala kwani jengo linalotumika sasa ni jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Sambamba na hilo, Mkurugenzi amesema kuwa, serikali pia imeridhia kutoa kiasi cha shilingi Bilioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali mpya ya Wilaya, hospitali ambayo si kwamba itakuwa mkombozi kwa wana mwanga tu, bali hata wilaya jirani zinazo izunguka wilaya ya Mwanga zitanufaika na ujenzi wa hospitali hiyo.

Akizungumzia suala la mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Mkurugenzi amesema kwamba, Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga mpaka sasa imefanikiwa kutoa mkopo kwa vikundi 48, mkopo wenye thamani ya Tsh. Milioni 269.8 kwa makundi yote matatu. Mikopo hii imetokana na jitihada kubwa iliyofanywa na Halmashauri katika kukusanya mapato ya ndani ambapo hadi kufikia kipindi cha robo ya pili 2021/2022 Halmashauri imefanikiwa kukusanya kiasi cha Bilioni moja na milioni miambili ishirini na moja. Ukusanyaji wa mapato ya ndani umekuwa ni chachu kubwa katika kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo, kwa mwaka huu wa fedha Milioni 344 imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo ya Wilaya.

Aidha, Mkurugenzi amewashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa ushirikiano wao mzuri walio uonyesha katika uanzishwaji wa mradi wa kimkakati wa Halmashauri, mradi wa kufyatua matofali. Akielezea manufaa ya mradi huo ambao ulianza kufanya kazi mwezi octoba 2021, Mkurugenzi alisema kuwa, mpaka kufikia sasa mradi umesha zalisha jumla ya matofali 62,178 na kufanikiwa kuingiza kiasi cha Tsh. Milioni 92. Amesema, mradi unaendelea vizuri na ameendelea kuomba Waheshimiwa madiwani pamoja na wananchi kuendelea kuunga mkono mradi huu kwa manufaa ya Halmashauri ya Mwanga na wananchi wake.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa