• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

VIJANA WILAYANI MWANGA WAASWA KUFUATA MAADILI NA UTAMADUNI WA MTANZANIA

Posted on: April 15th, 2023

Vijana wa Wilaya ya Mwanga wameaswa kufuata na kudumisha maadili na Utamaduni wa Mtanzania kwa kuhakikisha kwamba, wanakemea mila na desturi zisizofaa katika jamii na katika maisha yao ya ujana ya kila siku.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Ndg. Eliakimu E. Kimuto, aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye fainali ya kombe la pasaka lililo andaliwa na mdau wa michezo Ndg. Raymond Kyarua Abraham wa Mwanga.

Ndg. Kimuto amesema kwamba, vijana wanapaswa kukemea kwa nguvu zote, matendo maovu ambayo yamekuwa yakiibuka kwenye jamii zetu ikiwa ni matendo yaliyo kinyume na maadili ya mtanzania. Ameendelea kueleza kwamba, kwa sasa suala la ushoga linapaswa kukemewa kwa mbinu zote, huku vijana wakipaswa kuwa mstari wa mbele katika kukemea mambo ya ushoga. "Haipendezi wazazi wetu wakawaona vijana wao wakiiga tamaduni zisizo faa, kwani wakiwa kama wazazi wanaumia pale wanapo waona vijana wao wakiwa katika mwenendo usiofaa, amesema Ndg. Kimuto.

Sambamba na hayo, amewaasa jamii ya wana Mwanga, kuhakisha wanaupenda utamaduni waliolelewa nao, utamaduni ambao unaenzi tunu za taifa letu la Tanzania.

Naye mdau wa michezo Ndg. Raymond Kyarua Abraham, ambaye ndiye aliye andaa ligi hiyo ya pasaka Wilayani Mwanga, amewapongeza vijana walioweza kushiriki ligi ya Pasaka kwa kusema kwamba, michezo inaimarisha urafiki, inajenga umoja pamoja na kuimarisha afya ya mwili na akili.

Ligi hiyo ya Pasaka ilizishirikisha timu tano, ambazo ni Wakongwe FC, Reli Juu, Bodaboda, TRA na Jitimai. Timu zilifanikiwa kuingia fainali ni Wakongwe FC na Reli Juu, ambapo timu ya Wakongwe waliibuka washindi wa ligi hiyo kwa kuwafunga Reli Juu kwa mabao matano ya penati dhidi ya mabao matatu ya Reli Juu.

Ndg. Raymond amewaasa wadau mbalimbali wa michezo wa ndani na nje ya Wilaya ya Mwanga kuwekeza kwenye michezo kwa kusema kwamba, wadau wakijitokeza watawasaidia vijana wengi kutojihusisha na matendo maovu kama ngono uzembe, ambapo inaweza kupelekea kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa