• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

Posted on: March 15th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mhe. Abdallah Mwaipaya, amewakaribisha wananchi wa Wilaya ya Mwanga na wananchi wa Wilaya jirani kushiriki kwenye mapokezi ya kumpokea na kumkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango atakapokuwa kwenye ziara ya kikazi Wilayani Mwanga tarehe 21 Machi, 2024.

Mhe. Mwaipaya ameyasema hayo leo tarehe 15.03.2024 alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kusikiliza kero za wananchi wa kijiji cha Kagongo kata ya Lang’ata Bora. Amesema kwamba, Makamu wa Rais anategemea kutembelea na kukagua hatua ulipofikia mradi wa maji wa Same – Mwanga – Korogwe pamoja na kuongea na wanachi wa Wilaya ya Mwanga katika eneo la stand mpya. “Nitumie nafasi hii kuwaalika na kuwakaribisha wanachi wote wa wilaya ya Mwanga na wananchi wa wilaya jirani kwenye mapokezi ya kumpokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakapo tembelea wilaya yetu tarehe 21.03.2024”, Alisema Mhe. Mwaipaya.

Sambamba na hilo, Mhe. Mkuu wa Wilaya pia amewakaribisha wananchi wa Wilaya ya Mwanga kwenye sherehe za kuwasha Mwenge wa Uhuru zitakazofanyika katika uwanja wa Ushirika – Moshi tarehe 02 Aprili, 2024. Akiwahutubia wanachi wa kijiji cha Kagongo, Mhe. Mwaipaya alisema kuwa, baada ya sherehe za uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru, utakimbizwa Halmashauri zote za Mkoa wa Kilimanjaro na Mwenge wa Uhuru utaingia Wilayani Mwanga tarehe 07 Aprili, 2024. Katika hotuba yake kwa wananchi hao, alisema kwamba, wananchi wa Mwanga huwa ni washiriki wazuri sana kwenye sherehe zote za Mwenge wa Uhuru, kwa kila mwaka, hivyo anawaalika kushiriki katika matukio yote mawili ambayo ni sherehe za uzinduzi na sherehe za kukimbiza pamoja na kukesha na Mwenge Wilayani Mwanga tarehe 07 Aprili 2024.

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mwanga imekuwa ikifanya ziara za mara kwa mara. za kuwatembelea wananchi wake, na kusikiliza kero zao pamoja na kuzipatia utatuzi. Ziara hizi zimekuwa za manufaa makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuokoa gharama kubwa za kufika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kuwasilisha kero zao.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa