• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WANANCHI WA KARAMBANDEA WANUFAIKA NA SHIRIKA LA UHIFADHI WA MALI ASILI (WWF)

Posted on: December 1st, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Karambandea ambacho kipo kata ya Toloha Wilayani Mwanga, wameanza kunufaika na mradi wa shirikika la kimataifa la WWF shirika linalo jihusisha na uhifadhi wa wanyama pori na mazingira. Shirika la WWF limeanza mradi wake wa utafiti wa simba katika ukanda wa Tarafa ya Jipendea hususani katika kijiji cha Karambandea, kijiji ambacho kipo karibu kabisa na mbuga ya wanyama pori ya mkomanzi na mbuga jirani ya Tsavo Kenya.

Sambamba na uanzishwaji wa mradi huu, miongoni mwa manufaa ambayo mradi umeleta na unategemea kuendelea kuleta kwa wananchi wa Karambandea ni pamoja na ujenzi wa maboma ya kisasa ya kulaza mifugo ili isidhuriwe na wanyama aina ya paka kama simba, chui,duma, fisi nk. Manufaa mengine ambayo wananchi wa kijiji hicho wameanza kunufaika nayo ni mradi wa umeme wa sola ambapo mradi huu utasaidia katika kudhibiti na kupambana na wanyama wakali. Pia mradi umeanza kuleta manufaa kwa jamii hii kwa kuweza kujengewa Bwawa la kunyweshea mifugo, bwawa ambalo litakuwa msaada mkubwa wakati wa kiangazi.

Msimamizi wa mradi huo wa simba ambaye anahusika na usimamizi upande wa Tanzania na Kenya Prof.Noah Sitati ambaye alishiriki katika ziara ya kuuzindua mradi huo alisema, mradi huu utasaidia wanyama pori kuongezeka na watalii wataingia kwa wingi kupitia wilaya ya Mwanga. Pia mradi utawezesha kufunguliwa kwa lango la utalii kwa upande wa wilaya ya Mwanga kwenda mbuga ya wanyama ya Mkomanzi. Prof. Sitati pia amesema, hapo baadae mradi utawezesha kuanzishwa kwa miradi ya kuboresha nyasi kwa ajili ya malisho ya mifugo.

Naye Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Ndg. Abdllah Mwaipaya, amelishukuru shirika la WWF kwa mpango wake mzuri wa kuja na mradi wa utafiti wa simba hapa Wilayani Mwanga kwani eneo la Karambandea lina mgongano mkubwa na wa mara kwa mara kati ya wanyamapori na binadamu. Ameendelea kusema kwamba, mradi huo utasaidia utunzaji wa mazingira kwa asilimia kubwa, pamoja na kuinufaisha jamii ya wafugaji wa Karambandea na Tarafa ya Jipendea kwa ujumla.

Mhe. Mwaipaya pia ameishukuru jamii ya wananchi wa Karambandea kwa kukubali kupokea mradi huo kwani wananchi wa kijiji hicho wamekuwa wakikataa miradi mingi kutokana na uelewa mdogo waliokuwa nao awali kuhusu miradi. Amesema, wananchi hao kwa sasa wamepatiwa elimu vizuri na wameshaanza kuelewa umuhimu wa miradi katika maeneo wanayoishi.  

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa