• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WANANCHI WA MWANGA WAFURAHISHWA NA UJIO WA WAZIRI MKUU, AWAAHIDI MAJI YA UHAKIKA

Posted on: September 25th, 2021

Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewaahidi wananchi wa Wilaya ya Mwanga kuwa, wategemee kupata maji ya kutosha kutoka kwenye mradi mkubwa wa maji wa Mwanga - Same - Korogwe. Aliyasema hayo wakati alipotembelea mradi huo hapo jana na kujionea namna shughuli za mradi zinavyoendelea kuanzia sehemu ya chanzo cha mradi pamoja na sehemu ya kutibu maji.

Mradi wa Mwanga - Same - Korogwe ni mradi ulioanza toka Desemba, 2014 na sasa umefikia asilimia 64%. Akieleza sababu za kuchelewa kwa mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 262, Mhe. Waziri Mkuu alisema, ili mradi huo ukamilike unapitia hatua nne ikiwa ni pamoja na hatua ya kutengeneza chanzo, kutengeneza eneo la kutibu maji, kujenga visima na kulaza mabomba kwaajili ya kusambaza maji. Kutokana na kazi za maeneo haya manne kuwa kubwa, imechangia mradi kuchelewa kukamilika.

Katika hotuba yake, Mhe. Waziri Mkuu pia hakuacha kusemea vijiji ambavyo mradi umeanzia pamoja na vijiji ambavyo mradi utapita. "Wasimamizi wa mradi wahakikishe kuwa, vijiji vyote ambavyo vipo kwenye chanzo cha mradi pamoja na vile vijiji ambavyo mabomba yatapita vipatiwe maji" alisema Waziri Mkuu.

Mradi wa Mwanga - Same - Korogwe ni mradi mkubwa wa kimkakati, wenye thamani ya shilingi bilioni miambili sitini na mbili. Mradi huu utakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi zaidi ya 438,000 wa Wilaya za Mwanga, Same na Korogwe na utakuwa na uwezo wa kutoa maji masaa ishirini na nne kila siku.

Aidha, katika ziara yake hiyo, aliweza kukutana na mkandarasi aliyekuwa akisimamia mradi, mkandarasi ambaye mkataba wake ulivunjwa mwanzoni mwa mwaka huu. Mhe. Waziri Mkuu alimwagiza Waziri wa Maji kuwa, mkandarasi huyo arudi kazini ili aendelee na kazi na kumtaka mkabdarasi huyo aendelee na kasi ili mradi ukamilike mapema.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa