• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WATUHUMIWA SUGU WA UVUVI HARAMU WATIWA MBARONI

Posted on: January 4th, 2019

•NDOO 150 ZAKAMATWA

•MAGARI 2 NA PIKIPIKI 2 ZASHIKILIWA

Huku kukiwa bado kuna zoezi la operesheni ya uvuvi haramu katika bwawa la Nyumba ya Mungu, bado kuna baadhi ya wavuvi na wafanya biashara ambao wanajihusisha na shughuli za uvuvi haramu na biashara ya samaki wachanga katika bwawa hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Mhe. Aaron Yesaya Mbogho, ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, amesema, pamekuwepo na operesheni ya mara kwa mara katika bwawa hilo.

Akiwa anazungumzia zoezi la kuwakamata wahalifu waliokamatwa usiku wa kuamkia leo, ameeleza kuwa, zoezi la kuwakamata wahalifu hao limefanyika kuanzia saa nne usiku mpaka saa saba usiku. Ametabainisha kuwa, ofisi yake kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya pamoja na wataalam wa uvuvi wa Halmashauri, wamewakamata watuhumiwa sugu wa uvuvi haramu na wafanya biashara ya samaki wachanga watatu ambao ni, Godlizen B. Mfinanga, Juma Hassani Muharuma na Shafi B. Konde ambapo wengine walifanikiwa kukimbia. Watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa wamebeba ndoo 150 za samaki wachanga pamoja na nyavu haramu.

Pia katika operesheni hiyo wameweza kukamata magari mawili yote yakiwa ni aina ya pajero, moja likiwa na namba T 527 AEQ na lingine likiwa na namba T 210 ADF. Pia wamekamata pikipiki mbili zenye namba za usajili MC 546 CBR na MC 527 BPV.

Akizungumza kuhusu zoezi hili, Afisa Uvuvi Ndg. David Kabodo alisema, operesheni ya uvuvi haramu katika bwawa la Nyumba ya Mungu ni endelevu na watakwenda mpaka Wilaya ya Simanjiro husasani kwenye vijiji vinavyozunguka bwawa ili kuhakikisha kuwa, wavuvi haramu wanaokimbilia huko wanatiwa mbaroni na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Aidha, ofisi ya Mkuu wa Wilaya inaendelea kutoa wito kwa wananchi wa Wilaya zinazo zunguka bwawa hilo kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa serikali ili uvuvi haramu uweze kutokomezwa. Pia ofisi inaendelea kutoa shukrani kwa wananchi wanaoendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa pale wanapo ona vitendo vya uvuvi haramu katika maeneo yao.


Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa