• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

DC MWAIPAYA AZINDUA MIONGOZO YA ELIMU WILAYANI MWANGA

Posted on: September 20th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Mhe. Abdallah Mwaipaya, leo amezindua rasmi miongozo ya elimu kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga. Miongozo hiyo ambayo ilitolewa na Ofisi ya Rais TAMISSEMI, kwa ajili ya shule za Msingi na Sekondari, imezinduliwa kwa lengo la kuwawezesha wasimamizi wa masuala ya elimu na wadau wa elimu, kufahamu maudhui yaliyo katika miongozo hiyo kwa lengo la kuendelea kuinua taaluma ya wanafunzi katika nchi yetu.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa miongozo hiyo, Mhe. Mwaipaya amesema kwamba, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, imetoa miongozo mitatu ambayo ni Mwongozo wa Uteuzi, Mwongozo wa Changamoto za Elimu na Mwongozo wa Mikakati ya Kutoa Elimu Bora katika Shule za Msingi.

Katika hotuba yake, Mheshimiwa Mwaipaya amesema, miongozo hii, inakwenda kutatua changamoto mbalimbali zilizopo katika sekta ya elimu, kwani imejikita katika kuhakikisha kuwa, sekta inakuwa na viongozi bora wenye uadilifu, weledi utendaji na usimamizi mzuri.

Sambamba na hayo, Mheshimiwa Mwaipaya amesisitiza kuwa, miongozo hii inakwenda kusaidia utoaji bora wa elimu kwa wanafunzi wote wa sekondari na msingi, ikiwa ni pamoja na utatuzi wa changamoto kwa baadhi ya wanafunzi kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) kwa wakati, kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata chakula cha mchana shuleni, pamoja na uwepo wa miundo mbinu bora, wezeshi na rafiki kwa walimu na wanafunzi.

Aidha miongozo hii itawezesha uwepo wa ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi shuleni, itahakikisha kuwa wanafunzi wanaojiunga na darasa la kwanza wanakuwa wamepata elimu ya awali, pia itasaidia kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopenda kusoma masomo ya sayansi na michepuo ya sayansi katika shule za sekondari, alisema Mheshimiwa Mwaipaya.

Kwa upande mwingine, Mheshimwa Mwaipaya amewataka wadau wa elimu pamoja na wazazi wa wilaya ya Mwanga kuhakikisha kuwa, wanashirikiana kwa karibu na walimu wanaofundisha watoto wao ili kuweza kutekeleza miongozo hii kwa urahisi, ikiwa na pamoja na kuhakikisha kuwa wanatoa ushirikiano, katika utoaji wa chakula kwa ajili ya wanafunzi na uwepo wa michezo. “Naamini tukitoa chakula shuleni, hata utoro wa wanafunzi utakuwa haupo, hii ni pamoja na kuhakikisha michezo inakuwepo shuleni ili kupunguza utoro”, alisema Mheshimiwa Mwaipaya.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Bi. Mwajuma A. Nasombe, amesema kuwa, wadau wa elimu na wazazi, ni miongoni mwa watu muhimu sana katika Wilaya ya Mwanga, kwani wanao uwezo mkubwa wa kusaidia walimu na wanafunzi kuwa na mazingira bora ya kusomea na kujifunzia. Amewaasa na kuwaomba wadau wa elimu na wazazi kuhakikisha kuwa, wanaunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na utoro shuleni, uwepo wa chakula cha mchana na uwepo wa makazi bora ya walimu.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa