• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

KAENI KWENYE MAENEO YENU YA KAZI, ASEMA AFISA ELIMU MSINGI MWANGA

Posted on: December 7th, 2018

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Mwanga Bi. Mariana Mgonja, leo amefanya kikao kazi na wataalamu wake ambao ni Maafisa wa Idara ya elimu msingi, Waratibu Elimu Kata na Walimu Wakuu. Kikao hicho lengo lake kuu lilikuwa ni kuona changamoto zilizopo shuleni, namna ya kuzitatua na kuweka mikakati mizuri ya kitaaluma itakayo wezesha taaluma kupanda haswa kwa madarasa yenye mitihani, ambayo ni darasa la saba na darasa la nne.

Pamoja na changamoto mbalimbali zilizopo shuleni, Afisa Elimu amewaagiza walimu wakuu na waratibu elimu kata kuhakikisha kuwa, wanaishi kwenye maeneo yao ya kazi ili muda wote waweze kukabiliana na changamoto zilizopo. "Haiwezekani kituo chako cha kazi kiwe Mwanga halafu uishi Same". Amesema Afisa Elimu.

Katika kikao kazi hicho, Afisa Elimu kwa kushirikiana na Maafisa wa Idara yake, walimu wakuu na waratibu, waliweka mikakati ambayo wataisimamia kwa mwaka 2019 ili shule ziweze kufanya vizuri kwenye ufaulu. Baadhi ya mikakati iliyowekwa ni pamoja na kuhakikisha wanafunzi wanakula chakula cha mchana shuleni, kuwa na mtihani mmoja unaofanana wa nusu muhula na muhula kwa shule zote,  kudhibiti utoro, kuwa na mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, kutafuta walimu wa ziada na iwekwe mikakati ya namna ya kuwalipa na walimu wawe wanafundisha katika muda wa ziada.

Mikakati mingine ni kutoa motisha kwa wanafunzi na walimu wanaofanya vizuri, kumaliza silabasi kwa wakati, kuwa na michezo ili kupunguza utoro na kuifanya akili ichangamke, kuunda klabu za masomo na kuwapa wanafunzi kazi za nyumbani (home work).

Pamoja na hayo, Afisa Elimu amewaomba walimu kuonyesha ushirikiano ili kazi zifanyike kwa ufanisi mzuri. Pia amewataka wale wenye matatizo mbalimbali kama madai ya uhamisho waweze kufika ofisini kwake ili ajue anawezaje kuwasaidia katika kutatua changamoto zao. Pia amewataka walimu wakuu waendelee kushirikiana na jamii zinazo wazunguka na kuwashirikisha kwenye masuala yanayohusu shule ili waweze kuleta maendeleo ya shule zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGA KURA KWAAJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 July 04, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 03, 2025
  • Tangazo la nafasi 30 za kazi ya mkataba June 20, 2025
  • TANGAZO LA KAZI June 03, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC MUNKUNDA AONGOZA KONGAMANO LA MWAKA LA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (NGOs)

    June 18, 2025
  • WATUMISHI WA MWANGA DC WAPATIWA MAFUNZO YA E-UTENDAJI.

    June 19, 2025
  • MWANGA YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA

    June 16, 2025
  • MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    June 13, 2025
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa