• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFURAHISHWA KWA UKUWAJI WA VIWANDA WILAYANI MWANGA

Posted on: May 12th, 2023

Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, jana tarehe 11 Mei, 2023, ilitembelea na kukagua viwanda sita vilivyopo katika Wilaya ya Mwanga. Lengo la ziara hiyo lilikuwa ni kujionea namna ambavyo viwanda hivyo vinafanya kazi za uzalishaji, pamoja na kujifunza teknolojia zinazotumika katika kuendesha viwanda hivyo. Viwanda vilivyo tembelewa ni Kiwanda cha kokoto Kifaru, Kiwanda cha Katani Kisangara (Mahamed Enterprises) na Kiwanda cha Shaba Kiruru (Mega Copper). Vingine ni Kiwanda cha Maji Lambo (Mwanga Pure Drinking Water), Kiwanda cha Kifaru Biochem na kiwanda cha mikate (Kifaru Bakery and Confectionery).

Wajumbe wa Kamati hiyo, walisema kwamba, wanafurahishwa na uwepo wa viwanda vingi hapa Wilayani Mwanga, kwani vimekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi haswa vijana. Akiongea kwa niaba ya wajumbe wa kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Mhe. Innocent J. Msemo alisema kwamba, uwepo wa viwanda hapa wilayani, ni fursa nzuri kwa kutoa ajira, kukuwa kwa uchumi wa Mwanga na Taifa, pamoja na kuchochea maendeleo ya wazawa.

Aidha, Kamati hiyo, iliwaasa wamiliki wa viwanda Wilayani Mwanga kuhakikisha kwamba wanatunza mazingira vizuri ili kuepuka uchafuzi wa mazingira. Pia wamesisitizwa kuendelea kuongeza fursa za ajira haswa kwa wazawa.

Uwepo wa viwanda Wilayani Mwanga imekuwa ni chachu kubwa ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Viwanda vingi vimekuwa vikisaidia kuunga mkono ujenzi wa barabara, kuchangia ujenzi wa miundombinu ya Elimu, kutoa maeneo ya kilimo cha muda kwenye mashamba, ajira za muda mfupi na muda mrefu, mafunzo ya ujasiriamali, kujenga viwanja vya michezo na kutoa vifaa vya kujifunzia shuleni kama computer.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa