• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

MKURUGENZI MTENDAJI WILAYA YA MWANGA ATOA MSAADA KWA WANAFUNZI WALIO ATHIRIKA BAADA YA BWENI KUUNGUA MOTO

Posted on: September 16th, 2022

Ikiwa ni siku mbili zimepita baada ya bweni la wasichana wa shule ya Sekondari Nyerere iliyopo Wilayani Mwanga kuungua moto, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Bi. Mwajuma A. Nasombe, leo ametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na pesa taslimu kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi waliounguliwa na vitu vyao vilivyokuwa ndani ya bweni hilo.

Akiongea mbele ya wanafunzi wa shule hiyo, Bi. Nasombe alisema, msaada ambao ameuleta umetokana na ushirikiano mkubwa ulio onyeshwa na watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na timu ya wataalamu wa Halmashauri, Wakuu wa Shule, Waratibu Elimu Kata, Benki, Mheshimiwa Mbunge wa Mwanga pamoja na wadau wengine.

Miongoni mwa vitu vilivyonunuliwa na kukabidhiwa kwa wanafunzi hao ni pamoja na masanduku na kofuli zake zenye thamani ya Tsh. 750,500/=, mafuta ya kujipaka, taulo za kike, ndala, hijabu, vesti, nguo za ndani, masweta na vitu vingine vingi vyenye thamani ya Tsh. 1,270,000/= vya kuwawezesha kuishi maisha kama ya awali ikiwa ni pamoja na kuwapatia fedha taslimu kwa kila mmoja kwa ajili ya fedha za kujikimu katika mahitaji madogo.

Sambamba na michango hiyo, kiasi cha Tsh. 1,020,000/= kilikabidhiwa kwa Mkuu wa Shule hiyo Bi. Severina Mologa kwa ajili ya kuanza ukarabati wa bweni lililoungua. Akikabidhi mchango huo Bi. Nasombe alisema, kiasi hicho ni kianzio tu, kwani Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, watahakikisha kuwa bweni hilo linakarabatiwa ndani ya muda na wanafunzi waendelee kulitumia.

Wakati huohuo, Mbunge wa Mwanga Mhe. Tadayo Anania, aliweza kufika shuleni hapo na kutoa jumla ya mifuko 20 ya sementi kwa ajili ya kuunga mkono harakati za kuanza ukarabati. Mhe. Tadayo alisema kwamba, nje ya mchango huo, pia atawaletea madaftari wanafunzi wote waliopatwa na adha ya kuunguliwa na vitu vyao.

Shule ya sekondari Nyerere, bweni lake moja linalotumiwa na wasichana, liliungua moto siku ya jumatano tarehe 14 Septemba, 2022, wakati wanafunzi wakiendelea na masomo majira ya saa tatu asubuhi na kupelekea vitu mbalimbali vya wanafunzi kuungua. Vyombo vya ulinzi na usalama bado vipo kazini kuendelea kuchunguza chanzo cha moto huo, na watakapo maliza kazi yao, taarifa rasmi itatolewa kupitia mamlaka husika.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi 30 za kazi ya mkataba June 20, 2025
  • TANGAZO LA KAZI June 03, 2025
  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC MUNKUNDA AONGOZA KONGAMANO LA MWAKA LA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (NGOs)

    June 18, 2025
  • WATUMISHI WA MWANGA DC WAPATIWA MAFUNZO YA E-UTENDAJI.

    June 19, 2025
  • MWANGA YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA

    June 16, 2025
  • MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    June 13, 2025
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa