• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

MRADI WA MAJI WA SAME, MWANGA, KOROGWE WAANZA KWA KASI

Posted on: March 13th, 2023

Waziri wa Wizara ya Maji Mhe. Jumaa H. Aweso (Mb) amesema kwamba, Wizara yake itamheshimisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha kwamba, mradi wa Same, Mwanga Korogwe unakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kufaidi maji yatakayotokana na mradi huo.

Mheshimiwa Waziri ameyasema hayo leo alipotembelea mradi huo mkubwa wa maji ambao chanzo chake ni bwawa la Nyumba ya Mungu lilipo Wilaya ya Mwanga. Katika maelezo yake amesema, "Mheshimiwa Rais alishanipa maelekezo juu ya mradi huu, nami nasema kwamba, nitahakikisha Wizara yangu inamheshimisha Rais, ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati", alisema Mheshimiwa Waziri.

Pamoja na ziara yake hiyo, Mheshimiwa Waziri ameshuhudia utiaji saini wa mkataba kati ya Wizara na kampuni ya M A KHARAFI AND SONS ya Kuwait, kampuni ambayo imepewa jukumu la kumaliza kazi iliyokuwa imesalia kwa muda wa miezi 14.

Katika kuhakikisha kuwa sehemu ya mradi huo inakamilika ndani ya muda, Mheshimiwa Waziri ametoa maelekezo kwa mkandarasi na kwa wasimamizi wa mradi kutoka Wizarani kuhakikisha kwamba, wanatoa taarifa kila mwezi kwamba mradi umefika asilimia ngapi ya utekelezaji. Ameendelea kusema kwamba, kwa sasa hivi hatarajii kupata visingizio vyovyote kuhusu maendeleo ya mradi kwani fedha zote zilizokuwa zinadaiwa na wakandarasi zimeshalipwa.

Katika hotuba yake, pia amesema kwamba, vijiji vyote tisa vilivyopo katika eneo la chanzo cha maji vitapata maji kwani mpaka sasa usanifu wa kupeleka maji katika vijiji hivyo umeshafanyika.

Akizungumzia suala la ajira kwenye mradi huo, Mheshimiwa Waziri amesema, mbali na kazi zinazohitaji taaluma kwenye mradi, kuna kazi zingine ambazo hazihitaji taaluma, hivyo anatoa wito kwa mkandarasi kuhakikisha kwamba, anatoa ajira kwa vijana wa maeneo ambayo mradi unatekelezwa.


Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa