• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

Mtoto Anthony mwenye uwezo wa ajabu apata ufadhili

Posted on: April 9th, 2018

Mtoto Anthony Petro (11) wa Ngara Kagera, leo amekabidhiwa rasmi Wilayani Mwanga Kilimanjaro kwa mfadhili aliyejitokeza kwa ajili ya kumpatia ufadhili wa masomo ambapo atasoma mpaka darasa la saba.

Kabla ya makabidhiano hayo, mtoto Anthony, alipokelewa kwa maandamano yaliyojumuisha wanafunzi wa shule za Mwanga na wananchi wake ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan J. Bahama alifanya zoezi la kumkabidhi mtoto huyo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Ndugu Golden A. Mgonzo.

Maandamano ya kumpokea mtoto huyo yalienda mpaka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mwanga ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mwanga alimtambulisha Anthony kwa Mhe. Aaron Y. Mbogho ambaye ni Mkuu wa Wilaya na baadae kuongozana mtoto huyo hadi Ofisi ya Mkurugenzi.

Baada ya zoezi la kumtambulisha na kumkabidhi mtoto huyo kwenye Ofisi ya Mkurugenzi kumalizika, msafara ulielekea shule ya Amani Vumwe English Medium ambapo ndipo alipopatiwa ufadhili wa masomo.

Akizungumza kwa furaha baada ya kukabidiwa mtoto huyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga alisema, mtoto Anthony alikuwa ni mtoto wa maisha ya chini ila sasa yuko juu na akaendelea kumtia moyo kuwa ili azidi kuwa juu zaidi ni lazima ajiamini, awe na hofu ya Mungu, bidii katika kazi na masomo, nidhamu, tabia njema, kuwa na mahusiano mazuri na wenzake. Na endapo Atazingatia haya atazidi kuendelea kuwa juu na hatarudi chini.

Aidha Mkurugenzi baada ya husia wake kwa Anthony, alimkabidhi mtoto huyo kwa Afisa Elimu Msingi Ngd Allan Said na kwa Afisa Ustawi wa Jamii Ndg Alex Kameo na kuwasisitiza kuwa, wahakikishe wanashirikiana na uongozi wa shule ya Amani Vumwe ili mtoto huyo apate malezi mazuri.

Naye Meneja wa Shule ya Amani Vumwe, Ndg Isaka Msuya, akizungumza katika tukio hilo la kumpokea mtoto huyo, alisema, baada ya kumuona mtoto huyo kwenye mitandao ya kijamii alishawishika kumsaidia na ndipo alipochukua jukumu la kumfadhili mtoto Anthony. Ameahidi kumsomesha Anthony mpaka atakapo maliza masomo yake ya elimu ya msingi. Meneja huyo amewaomba wamiliki wa shule zingine kuwa sehemu ya utumishi katika jamii kwa kusaidia kuwasomesha wasiokuwa na uwezo.

Mtoto huyu alianza kupata umaarufu baada ya taarifa zake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zilizokuwa zimeambatana na video inayoelezea maisha halisi anayoishi yeye na familia yake ambapo tarehe 12 machi, 2018 mwandishi wa habari wa Sahara Media, Ndg Shabani Nassibu Nyamukama alitoa taarifa inayoelezea maisha halisi ya mtoto huyo na ndipo alipojitokeza Meneja wa Shule ya Amani Vumwe na kuahidi kumsaidia kielimu. Pamoja na mtoto huyu kuwa ni mdogo kiumri inaonekana ana uwezo mkubwa wa kupambanua mambo na ufadhili ambao ameupata itakuwa ni njia nzuri ya kumuwezesha kusonga mbele kimaisha.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa