• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

SERIKALI YALISHUKURU KANISA LA KKKT KWA MSAADA WA CHAKULA KWA WANANCHI WILAYANI MWANGA

Posted on: March 17th, 2023

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imetoa shukrani kwa uongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha kwa kugawa chakula bure kwa wananchi wa vijiji saba wilayani Mwanga.

Shukrani hizo zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, Bi. Mwajuma A. Nasombe ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mwanga kwenye zoezi hilo la kugawa chakula.

Akitoa shukrani zake kwa kanisa hilo, Bi. Nasombe amesema, analishukuru sana kanisa la KKKT na viongozi wake kwa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhakikisha kwamba, kanisa linashirikiana na serikali katika kukabiliana na tatizo la njaa. Katika shukrani zake hizo, pia ameishukuru serikali kwa kuleta tani 411 za mahindi ambazo zimeuziwa wananchi wa Mwanga kwa bei nafuu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Kanisa la KKKT, Mhe. Baba Askofu wa Dayosisi ya Mwanga, Chedieli E. Sendoro, amesema, anaishukuru sana Serikali kwa kuendelea kuwapa ushirikiano katika masuala mbalimbali pale kanisa linapohitaji msaada.

Pamoja na shukrani hizo, Mhe. Baba Askofu ameongoza zoezi la ugawaji wa vyakula mbalimbali kwa wananchi wa Kata ya Toloha. Katika hotuba yake amesema kwamba, msaada walioutoa haujaishia Toloha tu, bali umejumuisha jumla ya vijiji saba ambavyo ni Pangaro, Kiverenge, Karambandea, Simu Kizungo, Kwakoa, Kwakihindi na Kwanyange. Amesema kwamba, jumla ya Kaya 780 zimenufaika na msaada wa vyakula mbalimbali ikiwa ni tani 39 za mahindi, tani 15 za maharage, tani 8 za unga wa lishe na lita 3300 za mafuta ya kula.

Serikali Wilayani Mwanga, imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na mashirika pamoja na taasisi mbalimbali za umma na binafsi kwa manufaa ya kuhakikisha kwamba, wananchi wake, wanapata huduma muhimu na za msingi haswa za kibinadamu.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa