• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WILAYA YA MWANGA YAADHIMISHA MIAKA 59 YA MUUNGANO KWA KUPANDA MITI

Posted on: April 24th, 2023

Leo Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga imeadhimisha sikukuu ya Miaka 59 ya Muungano kwa kufanikiwa kupanda zaidi ya miti 200 katika eneo ambalo hospitali mpya ya Wilaya ya Mwanga inaendelea kujengwa. Sikukuu ya Muungano kwa mwaka huu imebebwa na kuli mbiu inayo sema “Umoja na Mshikamano Ndiyo Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu”.

Zoezi hilo la upandaji miti limeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mhe. Abdallah Mwaipaya kwa kushirikiana na watumishi mbalimbali wa umma, Viongozi wa Chama tawala, wananchi na wanafunzi.

Akiongea wakati wa zoezi hilo la upandaji miti Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema kwamba, suala la utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji ni ajenda kuu ya Kitaifa, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuhakikisha kwamba analinda na kutunza mazingira na vyanzo vya maji. Zoezi la upandaji miti katika Wilaya ya Mwanga ni zoezi ambalo ni endelevu, tutaendelea kupanda miti kwenye taasisi zetu za umma ili mazingira yaendelee kuwa mazuri, amesema Mhe. Mkuu wa Wilaya. Amewaasa wananchi kuhakikisha kwamba miti ambayo imepandwa leo na miti mingine ambayo ilikwisha pandwa awali katika eneo hilo la hospitali ya Wilaya, inaendelee kulindwa na kutunzwa vizuri.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema kwamba, kuna faida nyingi za utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na biashara ya hewa ukaa ambayo itasaidia katika kukuza mapato ya serikali. Faida nyingine ni pamoja na hali ya hewa nzuri, mvua za kutosha, vyanzo vya kudumu vya maji na mazingira bora ya viumbe hai.

Mhe. Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi wa Mwanga haswa wafugaji kuhakikisha kuwa wanalinda na kutunza mifugo yao vizuri, ili kuepuka kuingia kwenye mgogoro na serikali, pale mifugo yao itakapo haribu miti na mazingira haswa kwenye maeneo yote ambapo serikali imepanda miti na maeneo yote yaliyo hifadhiwa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Bi. Mwajuma A. Nasombe amesema kwamba, kwa mwaka huu, Halmashauri ya Mwanga imepanga kupanda miti zaidi ya elfu kumi. Zoezi hilo la upandaji miti lilisha anza ambapo kila shule na taasisi zingine za umma zimehimizwa kupanda miti ili kutunza mazingira.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huwa inaadhimisha sikukuu ya Muungano kila inapo fika tarehe 26 Aprili ya kila mwaka, lengo likiwa ni kumbukizi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo, Tanganyika na Zanzibar ziliungana mnamo tarehe 26 Aprili, 1964.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa