• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mwanga District Council
Mwanga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na rasilimali watu
      • Afya
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii na Uhusiano
      • Ujenzi na zima moto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali asili
      • Mazingira
      • Mamlaka ya Mji mdogo
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za Uvuvi
    • Fursa ya Madini
    • Fursa ya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za kisheria
    • Huduma za kuwawezesha wajasiria mali
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mipango mikakati
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Bajeti ya Halmashauri
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Habari

WILAYA YA MWANGA YAADHIMISHA SIKU YA KUPINGA VITENDO VYA UKATILI KWA WANAWAKE NA WATOTO

Posted on: November 28th, 2022

Katika kuelekea maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto, leo Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, kwa kushirikiana na taasi ya Yatosha Foundation ya Wilayani Mwanga, imeadhimisha siku ya kupinga vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto.

Maadhimisho hayo, ambayo yalianza kwa maandamano yaliyo ongozwa na, wanafunzi zaidi ya 500 wa shule za msingi Mramba, Kawawa na Lwami, yalipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mhe. Abdallah Mwaipaya katika uwanja wa C. D Msuya.

Maadhimisho ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto, ambayo yalibebwa na kauli mbiu inayosema “Kila Uhai Una Thamani, Tokomeza Mauaji na Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto”, yalilenga kufikisha ujumbe kwa jamii na kutoa elimu juu ya vitendo vya kikatili vinavyofanywa kwa wanawake na watoto. Vitendo hivi vimekuwa vikileta maumivu makali ya kimwili na kiakili kwa wahusika na hata kupelekea msongo wa mawazo kwa wanaofanyiwa vitendo hivyo.

Mgeni rasmi katika tukio hilo ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, amesema kwamba, kuna haja kubwa kwa jamii ya watu wa Mwanga, kuendelea kupatiwa elimu ya mara kwa mara juu ya umuhimu wa kulinda na kutetea haki za watoto pamoja na wanawake, ili, kuwaepusha na vitendo vya kikatili, ambavyo wamekuwa wakifanyiwa mara kwa mara. Amesisitiza kwamba, wazazi nao wahakikishe kuwa, wanatoa nafasi ya kuwasikiliza watoto wao, kwani watoto wengi wakifanyiwa vitendo vya kikatili, baadhi ya wazazi hawana muda wa kuwasikiliza.

Katika hotuba yake, Mhe. Mkuu wa Wilaya ameendelea kusema, elimu dhidi ya ukatili isiishie kutolewa na watu wachache tu, bali iendelee kutolewa kupitia taasisi na mashirika mbalimbali ya binafsi na serikali ili watoto waelewe haki zao za msingi na waweze kujua ni namna gani ya kuepuka au kutoa taarifa dhidi ya mambo ya kikatili ambayo wamekuwa wakifanyiwa nyumbani ama mtaani.

Aidha, Mkuu wa Wilaya, hakuacha kuzungumzia juu ya umuhimu wa chakula cha mchana shuleni kwa kusema, “Serikali ya Wilaya ya Mwanga itaendelea kuwaelimisha wazazi, juu ya umuhimu wa chakula cha mchana shuleni, na baada ya muda, wazazi ambao watakaidi, Serikali itabidi iwachukulie hatua kwasababu, suala la kumnyima mtoto chakula cha mchana, ni sehemu ya unyanyasaji na ukatili” Amesema Mkuu wa Wilaya. Ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Bi. Mwajuma Nasombe kwa kusema, shule zote za Wilaya ya Mwanga zianzishe Club maalum za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kwani hii itasaidia kubaini mambo mengi ya kikatili wanayofanyiwa watotoi na namna ya kukababiliana nayo.

Maadhimisho ya siku ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, ni zoezi la kitaifa ambalo lilianza toka tarehe 25 Novemba, 2022, na yataazimishwa kwa  muda wa siku 16 ambapo, hitimisho kitaifa itakuwa tarehe 10/12/2022.

Matangazo

  • Tangazo la kazi April 17, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira February 21, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA February 16, 2025
  • Nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ajira January 30, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KARIBUNI TUMPOKEE MAKAMU WA RAIS – DC MWAIPAYA

    March 15, 2024
  • SERIKALI YAIPATIA SHULE YA MSINGI MWERO MILIONI 178.3

    October 12, 2023
  • MHE. TADAYO ATOA PONGEZI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO, ASEMA WILAYA INA VIONGOZI SAHIHI

    September 20, 2023
  • KIKUNDI CHA UTAMADUNI KUTOKA MWANGA KIMEULETEA MKOA WA KILIMANJARO USHINDI KWA AWAMU YA PILI MFULULIZO

    August 27, 2023
  • Tazama Yote

Video

Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATANGAZO
  • MIONGOZO
  • MFUMO WA USAJILI WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI (PREM)
  • Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Huduma za Afya
  • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Maktaba ya Picha
  • Kuomba kibali cha kusafiri nje ya nchi

Viunganishi Linganifu

  • PlanRep
  • Tovuti ya Ikulu
  • UTUMISHI
  • FFARs
  • Tovuti ya Wakala wa Serikali ya Mtandao
  • OR-TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga

    Sanduku la Posta: 176 Mwanga,Kilimanjaro

    Simu ya Mezani: +255 272974343

    Namba ya Simu: +255 272974343

    Barua Pepe: ded@mwangadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

hatimiliki ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga . Haki zote zimehifadhiwa